Mmea wa Mlonge- "Moringa Oleivera"



Umewahi kuusikia au kuuona mmea uitwao Mlonge? Au kwa lugha ya kilatini "Moringa Oleivera"? Binafsi niliwahi tu kuusikia na kwa bahati nzuri hivi majuzi nilibahatika kuuona. Mmea unaoonekana pichani wenye shina kubwa ndio Mlonge wenyewe kwa mujibu wa aliyenionyesha kwani mimi sikuwahi kuuona kabla.

Mmea huu ni dawa na unaaminika kutibu magonjwa mengi yawasumbuayo binadamu pengine hata na wanyama wengine. Majani yake,matunda yake,magome yake,maua na mizizi hutumika kama dawa, kila sehemu ya mti kwa umuhimu wake.

Inasemekana matunda yake yanatumika kama mboga kwa kukatakata kama kabichi na majani yake pia hutumiwa kama mboga kwa kupika kama mchicha. Majani yake hutibu magonjwa mbalimbali na kuongeza virutubisho vya mwili.

Maganda(magome) ya Mlonge husaidia kusafisha maji(water treatment).

Mizizi hutumika kutibu watu walio na malaria sugu au watu wanaopata homa ya usiku au wanaotiririka sana jasho wakati wa homa. Mizizi hutumika kwa kusaga unga wake na kutumia kijiko cha chai mara tatu kwa siku.

Kwa mujibu wa nilikodesa,mmea huu hutibu magonjwa mengi kama shinikizo la damu,kupooza viungo au kufa ganzi,homa ya matumbo(typhoid),kuwashwa mwili,vidonda vya tumbo,malaria sugu, enia, upele n.k. Ni magonjwa mengi yaliyoorodheshwa hadi na ukimwi. Sasa sijui ilikuwa ni kutaja tu magonjwa yote yaliyopo au vipi,mimi sijui.


Dozi ya Ukimwi.
Kwa mujibu wa desa lililo na maelezo ya mmea wa mlonge, dozi ya ukimwi ni kutumia unga wa majani kijiko cha chai mara tatu kutwa kwa muda wa siku arobaini na tano sawa na wiki sita. Pia mgonjwa anatakiwa kutafuna mbegu tatu mara tatu kwa muda wa siku arobaini na tano sawa na wiki sita.

Unahamasishwa na kushauriwa angalao nyumbani kwako uwe na mashina kadhaa ya mmea huu kwa matumizi yako.

Comments

Fadhy Mtanga said…
Bonge la somo. Ndo raha ya blog.
Wow!!!
Kumbe tuna tabibu mbalimbali, za asili na zisizo na madhara kama ya vidonge vya makemikali na bado tunapuuza.
Nimekuwa nikiusikia huu mmea lakini sijawahi kuona na wala kujua kwa undani matumizi yake.
Shukrani saana Kaka kwa maelezo haya ya ndani juu ya mti huu.
Baraka kwako
Ama kweli kublog ni kuzuri ni zaidi ya kwenda shule. Nilikuwa sijui kabisa juu ya huu mti. Ahsante sasa kakangu!!
Albert Kissima said…
Zamani watu walikuwa wakijitibu kwa dawa za asili(miti shamba) na karibu kila mtu alikuwa akijua miti ambayo ni dawa na ni kwa ajili ya ugonjwa gani. Leo hii dawa za asili zimedharauliwa na zinapewa msisitizo mdogo.

Dawa hizi hazijapewa msisitizo wa kutosha kwa sababu pia ya ubinafsi. Wakati zamani wazee walikuwa wakiwaonyesha watoto wao miti ipi ni dawa na ipi si dawa,leo hii utaratibu huo haupo na wale wajuao miti ambayo ni dawa wamekuwa wasiri kwani kwa sasa dawa za miti shamba ni ajira za watu. Wanahofia wakisema ni majani yapi au ni mti upi unaotibu malaria basi watakuwa wamekosa soko.
Bennet said…
Niliuongelea vizuri kwenye blog yangu, nitembelee
Albert Kissima said…
Nashukuru ndugu Bennet,nafurahi kusikia hivi na nitafika hapo kijijini kwako nipate mengi zaidi kuhusiana na mti huu.
Evarist Chahali said…
Hi Albert,asante kwa comments zako pale bloguni kwangu.Kwa bahati mbaya sijui nini kimetokea,siwezi kujibu comments.Natafuta ufumbuzi.Kazi njema ndugu yangu
Albert Kissima said…
Hi kaka Evarist,mimi cjambo na naendelea vyema.Naamini ufumbuzi utapatikana na mambo yatakwenda vizuri. Nakushukuru na we kwa kunitembelea. Karibu tena na nikutakie kila lenye kheri.
Anonymous said…
The information were very helpful for me, I've bookmarked this post, Please share more information about this
Thanks
Unknown said…
tunapenda watu wa namana hii wanaweza kutoa elimu za namana hii kwani uliwengu tulionao wazungu kama wametuloga ili tuwe tegemezi kwa viwanda vyao ,wakati wao tiba hizo huwa hawazigusi huku wakitumia malighafi kutokana na miti yetu,sasa ni wakati wa kuamka na kujua baraka tulizonazo,kutokana na miti,matunda na vyakula ,cha msingi ni wataalamu mtusaisidie jinsi ya kutumia
mbarikiwe
Unknown said…
kama mmea huu unatibu,Nitachukua sehemu mbalimbali za mmea huu na kuzichuguza kwanza kwa kutumia wataalamu tulio nao hapa muhimbili.
Unknown said…
It will good to have s scientific research of Mronga. I believe it will be helpful to everybody esp regarding the dosage. Blessings to this blog.
Unknown said…
It will good to have s scientific research of Mronga. I believe it will be helpful to everybody esp regarding the dosage. Blessings to this blog.

Popular posts from this blog

Mambo Makuu Manne ya Kuzingatia ili Kufanya Upimaji Endelevu Wenye Tija

Mambo Muhimu ya Kuzingatia Katika Kuboresha na Kuongeza Ufanisi wa Shule.

Kubadilika kwa Mitaala: Walimu na Wanafunzi Wabadilike kwa Namna Gani?