Posts

Showing posts from March, 2010

Mmea wa Mlonge- "Moringa Oleivera"

Image
Umewahi kuusikia au kuuona mmea uitwao Mlonge? Au kwa lugha ya kilatini "Moringa Oleivera"? Binafsi niliwahi tu kuusikia na kwa bahati nzuri hivi majuzi nilibahatika kuuona. Mmea unaoonekana pichani wenye shina kubwa ndio Mlonge wenyewe kwa mujibu wa aliyenionyesha kwani mimi sikuwahi kuuona kabla. Mmea huu ni dawa na unaaminika kutibu magonjwa mengi yawasumbuayo binadamu pengine hata na wanyama wengine. Majani yake,matunda yake,magome yake,maua na mizizi hutumika kama dawa, kila sehemu ya mti kwa umuhimu wake. Inasemekana matunda yake yanatumika kama mboga kwa kukatakata kama kabichi na majani yake pia hutumiwa kama mboga kwa kupika kama mchicha. Majani yake hutibu magonjwa mbalimbali na kuongeza virutubisho vya mwili. Maganda(magome) ya Mlonge husaidia kusafisha maji(water treatment). Mizizi hutumika kutibu watu walio na malaria sugu au watu wanaopata homa ya usiku au wanaotiririka sana jasho wakati wa homa. Mizizi hutumika kwa kusaga unga wake na kutumia kijiko cha chai

Popular posts from this blog

Mambo Makuu Manne ya Kuzingatia ili Kufanya Upimaji Endelevu Wenye Tija

Mambo Muhimu ya Kuzingatia Katika Kuboresha na Kuongeza Ufanisi wa Shule.

Kubadilika kwa Mitaala: Walimu na Wanafunzi Wabadilike kwa Namna Gani?