Posts

Showing posts from January, 2017

Uwezo wa Kujiajiri na Kuajirika Una Uhusiano na Namna za Ujifunzaji: Wanafunzi Wanahitaji Ujifunzaji Unaochochea Udadisi.

Image
  Picha Kutoka kwenye Video ya Wanafunzi wa Shule Wildwood IB World Magnet wakitumia mfumo wa ujifunzaji wa Udadisi. Video hii unaweza kuitazama hapa . Kati mwaka 2005 hadi 2007, Tanzania ilibadili mitaala kutoka kwenye mtazamo wa Mwalimu kama chanzo cha maarifa hadi ile ya Mwanafunzi kama kiichi na chanzo cha ujifunzaji wake. Mabadiliko haya yalihusisha shule za msingi, sekondari na Vyuo vya Ualimu.   Mabadiliko ya mitaala yalilenga kuandaa wahitimu watakaoweza kukabiliana na soko la ajira, kuweza kujiajiri, kuajirika, kuendana kasi ya mabadiliko ya kiteknolojia, kiuchumi na kijamii ikiwa ni pamoja na kukabiliana na kutatua changamoto zinazokabili jamii zinazowazunguka. Kwa bahati mbaya sana, haijakuwa wazi kama kumekuwa na mabadiliko yoyote ya mitaala kwenye elimu ya Juu. Pengine hali hii inaweza kuchangiwa na ukweli kuwa, mitaala ya vyuo vikuu bado haijaunganishwa pamoja. Hata hivyo, Tafiti nyingi zilizofanyika nchini Tanzania, zinaonesha kuwa, mitaala hiyo h

Popular posts from this blog

Mambo Makuu Manne ya Kuzingatia ili Kufanya Upimaji Endelevu Wenye Tija

Mambo Muhimu ya Kuzingatia Katika Kuboresha na Kuongeza Ufanisi wa Shule.

Kubadilika kwa Mitaala: Walimu na Wanafunzi Wabadilike kwa Namna Gani?