Posts

Showing posts from May, 2010

Mwonekano wa kilele cha mlima Kilimanjaro kulingana na mahali mtu alipo mkoani Kilimanjaro.

Image
Muonekano wa kilele cha mlima Kilimanjaro kwa hapa mkoani Kilimanjaro hutegemea na mahali unapouangalia mlima huu. Wilaya ya Moshi(mjini na vijijini), Rombo, na baadhi ya maeneo wilayani Hai, (Siha, Mwanga na Same sijawahi ku-view mlima Kilimanjaro hivyo sitaweza kuzungumzia mwonekano wa kilele cha Mlima kwa sasa. Pengine mwonekano hautatofautiana na wa Rombo au Moshi) kilele cha mlima huonekana kama jinsi picha inavyoonyesha hapo juu. Kwa baadhi ya maeneo kama Masama wilayani Hai na baadhi ya maeneo mkoani Arusha yanayopakana na mkoa wa Kilimanjaro. mwonekano wa kilele cha mlima ni tofauti kwani pale juu kabisa kunaonekana kuna bonde, kiasi kwamba mtu aliyeko Masama N'guni mathalani, akiambiwa achore kilele cha mlima kwa kadiri ya namna akionavyo kilele, atachora kama kinavyoonekana kwenye picha hapa chini. Nashindwa kuelewa ni kwa nini kilele ambacho ni "Iconic" ndicho ambacho huonyeshwa na hutumika zaidi kwenye picha na maonyesho mengi yahusuyo mlima huu. Kama sikupat

Uyoga huu wa Ajabu! hatua ya awali kabisa katika uotaji wake.

Image
Hii ndio hatua ya awali kabisa ya uotaji wa Uyoga niliouelezea katika posti niliyoipa kichwa cha habari "Uyoga huu wa Ajabu". Hatua hii ya awali kama inavyoonekana, ina umbo kama la kiazi mviringo. Ni ligumu sana na ndani kuna layer mbili,moja ya rangi nyeusi na nyingine ni nyekundu. Rangi hii nyekundu bila shaka ndio inayokuja kuwa rangi ya uyoga na hii layer nyeusi ndiyo hasa inayokuja kutanda kwenye tip ya uyoga na ndio hasa iletayo harufu mbaya. Kadiri ya uyoga huu unavyozidi kukua ndivyo na umbo hili kama la kiazi mviringo linavyozidi kupungua(bila shaka sehemu kubwa ya kilichohifadhiwa ndani ni chakula kisaidiacho ukuaji wa uyoga huu). Baada ya uyoga kukua,sehemu ya nje ya umbo hili kama kiazi mviringo ambayo ni nyeupe, kama picha inavyoonyesha, huonekana kama ngozi na huwa laini ambapo ile sehemu ya ndani iliyokuwa ngumu, inabadilika na kuwa maji mazito. Ni hayo kwa leo niliyokukusanyia ndugu msomaji kuhusiana na uyoga huu mimi niuonao wa ajabu. Wapo wengi kama mimi,

Popular posts from this blog

Mambo Makuu Manne ya Kuzingatia ili Kufanya Upimaji Endelevu Wenye Tija

Mambo Muhimu ya Kuzingatia Katika Kuboresha na Kuongeza Ufanisi wa Shule.

Kubadilika kwa Mitaala: Walimu na Wanafunzi Wabadilike kwa Namna Gani?