Tule papai kivingine kabisa.

Papai bichi linaweza kutumika kama mboga.

Twendeni jikoni pamoja. Hata wanaume tunaweza, eti haturuhusiwi kuingia jikoni! Mke akiugua au akisafiri!
Twende pamoja.

1. Chukua mapapai yako mabichi yaliyokomaa ila bado kuiva.

2. Yaoshe, kisha yachonge vizuri halafu uyaoshe tena kwani yatakuwa na utomvu.


3. Yakwangue na kikwaruzio cha karoti, hapo utapata saizi ndogo ndogo kama wakati unapokwaruza karoti. Baada ya hapo, chemsha kwa muda mfupi na maji kidogo, kisha epua.


5. Kaanga kitunguu pembeni kisha weka nyanya kulingana wingi wa mboga zako, pia na karoti kama zipo, acha mchanganyiko huu uive vizuri mpaka kupata rojo ya nyanya.


6.Weka mchemsho wako wa mapapai kisha, changanya vizuri na acha mboga yako iive vizuri, pia usisahau kuweka chumvi kwa kadiri ya kipimo chako.

Kwa wale wanaoweza kupata mapapai, wajaribu kupika mboga hii, ni tamu sana.

Nimtakie kila mmoja atakayesoma hapa wakati mzuri na muwe na furaha kila sekunde ya maisha yenu.

Comments

Asante kwa hii mboga mpya ya papai. Nitakapofika tena huko nyumbani nitajaribu. Kwani huku ni bei sana. Papai moja ni shilingi 3000/=
Albert Kissima said…
Pole sana dada Yasinta, hakika mapapai huko ni ghali sana!
Karibu Moshi huku mapapai bure kabisa.
Asante sana Kissima Itabidi nije huko Moshi. kwani hali ya hewa ya huko itapatani nami na ntakula mapapai mengi.
Albert Kissima said…
Karibu sana dada Yasinta.
mumyhery said…
papai bichi!!! sijui ntalipata wapi jamani, afadhali ungesema la kuiva labda nigepata hata la kopo
Albert Kissima said…
Usihofu dada Mumyhery, siku ukirudi huku nyumbani utaandaa mboga hiyo ya papai.
Nakushukuru kwa kukitembelea kibaraza changu, karibu tena na tena.
Anonymous said…
Jtgt
Kwanza nishukuru kwa kututakia wakati mzuri. Ni baraka saana kupata baraka toka kwa watu wema kama wewe.
Pili nashukuru kwa "maungo" haya ambayo nikijaaliwa kulinyaka hilo papai bichi itakuwa "muswano"
Blessings
Serina said…
Nimesoma papai bichi nikafikiria biriani... nami nitajaribu.
Albert Kissima said…
Ni papai bichi dada Serina, ambalo ganda lake halijakuwa la njano,bado la kijani kabisa. Jaribu, halafu utaniambia mboga hiyo jinsi ilivyo nzuri.
Kissima upo mzima naona umepotea kweli?
Albert Kissima said…
Mimi sijambo dada Yasinta,mimi mzima wa afya.
Majukumu fulani fulani tu yamenitinga,
lakini tupo pamoja.

Popular posts from this blog

Mambo Makuu Manne ya Kuzingatia ili Kufanya Upimaji Endelevu Wenye Tija

Mambo Muhimu ya Kuzingatia Katika Kuboresha na Kuongeza Ufanisi wa Shule.

Kubadilika kwa Mitaala: Walimu na Wanafunzi Wabadilike kwa Namna Gani?