Dunia sasa imekuwa kama kijiji, au niseme kamtaa fulani hivi.Ikidhaniwa kama ni mduara basi naweza kusema kuwa kipenyo chake kimepunguzwa kwa kiwango kikubwa kabisa. Twashukuru, ukuaji wa teknolojia ya intaneti umefanikisha hili kwa kiasi kikubwa kabisa.
Mwanzoni, miaka kadhaa iliyopita teknologia ya intaneti ilikuwa ni kwenye kompyuta tu, lakini hivi sasa huduma hii ipo hadi kwenye simu za viganjani.Uwezo wake wa kufanya kazi unategemea na uwezo wa simu yenyewe. Unaweza kutuma email,kupokea jumbe za email, online chat,unaweza kufungua tovuti yoyote na ukasoma vilivyomo na mambo mengine mengi yahusuyo intaneti. Kwa mantiki hii hakuna atakayeshangaa nikisema inawezekana kutembea huku ukiblog, yawezekana kupitia blogs za wadau mbalimbali kupitia mtandao wa simu. Waweza kuweka posti, hata kuanzisha blogs kupitia mtandao huu wa simu. Inawezekana. Unaweza kuongeza ufanisi wa simu kwa kutumia phone applications ambazo zinaonekana ni msaada mkubwa hasa kwa upande wa blogs. Najua wapo wanaofahamu matumizi niliyoyataja ya intaneti ktk simu, pengine hii ni kwa manufaa ya wasiofahamu.
Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo huduma ya intaneti kupitia komputa bado ni ya hali ya chini sana na kupata huduma hii kwa uzuri bado ni gharama sana, watu wengi hawawezi kumudu kulipia gharama hizo. Lakini kwa kiasi fulani wapo watu wengi wenye simu na zenye uwezo wa intaneti na kwa bahati mbaya hawana ufahamu wa kuitumia huduma hiyo. Wanaona tu ufahari wa kuwa na simu ya gharama.
Kwa kutumia phone application,(kiwezesha simu) sina hakika kama ndio kiswahili chake, iitwayo OPERA MINI, mtu anaweza kupitia blogs na mambo mengine kwa uzuri kabisa, ila yategemea na uwezo wa simu. Ni phone application nzuri ambayo mbali na blogs, mambo mengine lukuki kama kusoma mambo yahusuyo masomo ya darasani kwenye intaneti, kupitia magazeti mengine ya habari mbali na blogs na mambo mengine mengi. Ina uwezo wa kupunguza pages kwa kiasi kikubwa, yani mambo yaliyotakiwa kuwepo kwenye pages tano, yanaweza kuwa kwenye page moja. Application hii ilikuweza kuitumia huna budi kui-download ktk simu. Kuna versions nyingi, lakini Opera mini 4.2 na operamini 5 beta ni versions za hivi karibuni na zina uwezo mkubwa. Yeyote atakayependa kuwa na application hii katika simu yake aielekeze hapa, Mini.opera.com.
Ipo phone application nyingine iitwayo SNAPTU. Nayo ni nzuri, inamwezesha mtu kupitia yaliyoandikwa bloguni, lakini bila ya kuwa na uwezo wa kuchangia.
Si lengo langu kutangaza miradi hii ya watu, bali ni katika kuangalia ni kwa namna gani watu wengi (hususani watanzania) wataweza kuwa na uwezo wa kupitia blogs na kupata yale yanayojiri humo. Pengine hatua hii yawezekana ikawa ni msaada mkubwa na ikafanikisha kuongeza idadi ya wazifahamuzo na pia wazisomazo blogs.
Pia kwa yeyote mwenye ufahamu zaidi kuhusu namna nzuri zaidi ya kuweza kuzipitia blogs kwa kutumia mtandao wa simu anaweza kuweka bayana ili hatimaye mpaka kule Uru Mruwia, Shimbwe, Ngudu, Bumbuli na kwingineko blogs ziweze kupaza sauti.
Saturday, November 28, 2009
Saturday, November 7, 2009
Ukosefu wa UZALENDO, sumu ya Mafanikio Tanzania.
Tanzania ni nchi ambayo imebarikiwa kwa kuwa na rasilimali za kutosha kabisa ambazo zikitumika vizuri zinaweza kubadilisha hali mbaya ya uchumi na umasikini tulionao watanzania tulio wengi.
Hali ya "umimi" kwa viongozi wengi wa serikali inakithiri kila kukicha, hili lajidhihirisha kwa namna watu wanavyotumia kila mbinu kupata uongozi kuliko kutafakari hali halisi ya watanzania.Watu wanazitafuta nafasi za uongozi kwa manufaa yao binafsi na kulisahau taifa. Tujiulize viongozi wastaafu mathalani maraisi,wana mchango gani baada wao kuachia ngazi? Wengine wanasahaulika kabisa kama walishakuwa maraisi!Hivi baada ya Nyerere kung'atuka alipotelea mitini kabisa? Umimi, ukosefu wa "uzalendo" kwa viongozi wetu ni tatizo kubwa na ni sumu ya maendeleo.
Wananchi nasi twahitaji kuwa wazalendo pia.Yashangaza sana,tena sana kwa baadhi ya wananchi kushabikia chama kuliko uwezo wa mgombea ktk uongozi. Utamsikia mtu anasema mimi ni CCM damdam kwani kila mwaka inashinda tu,hawashindwi hawa,hata kama ni kwa kuiba kura ilimradi wanashinda! Yasikitisha ushabiki wa mchezo wa mpira wa miguu ndio watumika hata kwenye siasa,yani ni sawa na mtu aseme kuwa ametokea tu kuipenda Simba sport club kwa sababu mpaka sasa ktk msimu huu wa ligi inashinda tu. Utaratibu huu kwenye michezo ni sawa kabisa lakini si kwenye siasa.Utaratibu huu wa ushabiki wa michezo unapoingizwa kwenye siasa, ni hatari na ndio unachangia sana kuchagua viongozi wasio na uzalendo na walio na umimi uliokithiri na ambapo ni matokeo ya wananchi wasio na uzalendo.
Misingi ya uzalendo miongoni mwetu sisi kama wananchi na miongoni mwa viongozi wetu ni muhimu sana kwa maendeleo chanya ya Taifa letu.
Hali ya "umimi" kwa viongozi wengi wa serikali inakithiri kila kukicha, hili lajidhihirisha kwa namna watu wanavyotumia kila mbinu kupata uongozi kuliko kutafakari hali halisi ya watanzania.Watu wanazitafuta nafasi za uongozi kwa manufaa yao binafsi na kulisahau taifa. Tujiulize viongozi wastaafu mathalani maraisi,wana mchango gani baada wao kuachia ngazi? Wengine wanasahaulika kabisa kama walishakuwa maraisi!Hivi baada ya Nyerere kung'atuka alipotelea mitini kabisa? Umimi, ukosefu wa "uzalendo" kwa viongozi wetu ni tatizo kubwa na ni sumu ya maendeleo.
Wananchi nasi twahitaji kuwa wazalendo pia.Yashangaza sana,tena sana kwa baadhi ya wananchi kushabikia chama kuliko uwezo wa mgombea ktk uongozi. Utamsikia mtu anasema mimi ni CCM damdam kwani kila mwaka inashinda tu,hawashindwi hawa,hata kama ni kwa kuiba kura ilimradi wanashinda! Yasikitisha ushabiki wa mchezo wa mpira wa miguu ndio watumika hata kwenye siasa,yani ni sawa na mtu aseme kuwa ametokea tu kuipenda Simba sport club kwa sababu mpaka sasa ktk msimu huu wa ligi inashinda tu. Utaratibu huu kwenye michezo ni sawa kabisa lakini si kwenye siasa.Utaratibu huu wa ushabiki wa michezo unapoingizwa kwenye siasa, ni hatari na ndio unachangia sana kuchagua viongozi wasio na uzalendo na walio na umimi uliokithiri na ambapo ni matokeo ya wananchi wasio na uzalendo.
Misingi ya uzalendo miongoni mwetu sisi kama wananchi na miongoni mwa viongozi wetu ni muhimu sana kwa maendeleo chanya ya Taifa letu.
Sunday, October 18, 2009
Nimechoka!
Sijachoka kuelimisha, sijachoka kuelimishwa,sijachoka kuburudisha!
Lakini!
Nimechoka na ubabaishaji wa huduma za serikali.BiMA YA AFYA kwa mfano,utaambiwa ugonjwa huu bima ya afya haiwezi kutibu, dawa hizi,kwa bima ya afya hutaweza kuzipata, walazimika kwenda kununua! Msaada wake nini sasa! Kweli nimechoka!
Nimechoka na sera nzuri na zenye mvuto kwa kuandikwa na kusemwa tu pasipo kuwa na utekelezaji.Sitamani kuzisikia wala kuzisoma popote tena! Miaka arobaini na saba na bado hatuoni nafuu! Mimi nimechoka kwa kweli!
Nimechoka kumpa kura ya kwenda kula mbunge wangu.Huwa namwona wakati wa chaguzi tu. Nikijaribu kufikiria kwa kipindi cha miaka yote ya ubunge kanifanyia nini ambacho atakapokuja tena kuomba kura atajivunia nacho na wananchi watafurahi kumwona tena, sikipati.Binafsi nimechoka! Nimechoka!
Umeme wakosekana masaa ishirini na matano na si mara moja kwa wiki!.Hakika haya ni masihara! Kwa hali hii lazima ningechoka tu!
Na nimeshachoka.
Ni kweli chama kimoja chashinda kwa halali miaka nenda uje? Kwa hali iliyopo, ni kweli watanzania ndio huwa wanakipigia kura! Ubabaishaji, rushwa, ufisadi,umasikini, kujengewa dhana ya kuwepo kwa amani lakini ni fujo na vurugu kila kukicha!Hivi, Yote haya kwa watanzania ni wimbo mzuri unaotufurahisha au ni nini?
Nimechoshwa! Nimechoshwa! Na kweli nimechoka.
Hivi,
kinachotuchosha watanzania ni, chama, mtu, watu au ni serikali? Au ni mfumo wa utawala?
Kwa vyovyote vile nimechoshwa na kweli nimeshachoka!
Kifaranga niliyetelekezwa, najitafutia kula mwenyewe, pori nijualo, kwa namna niwezayo. Kweli kwa hali hii maasi yatakwisha! Hali kama hizi si vichocheo tu vya matukio kama mauaji ya albino,wizi wa mabenki,uporaji, watu kuvamiwa majumbani na matukio mengine lukuki dhidi ya binadamu?
Binafsi nimechoka!
Lakini!
Nimechoka na ubabaishaji wa huduma za serikali.BiMA YA AFYA kwa mfano,utaambiwa ugonjwa huu bima ya afya haiwezi kutibu, dawa hizi,kwa bima ya afya hutaweza kuzipata, walazimika kwenda kununua! Msaada wake nini sasa! Kweli nimechoka!
Nimechoka na sera nzuri na zenye mvuto kwa kuandikwa na kusemwa tu pasipo kuwa na utekelezaji.Sitamani kuzisikia wala kuzisoma popote tena! Miaka arobaini na saba na bado hatuoni nafuu! Mimi nimechoka kwa kweli!
Nimechoka kumpa kura ya kwenda kula mbunge wangu.Huwa namwona wakati wa chaguzi tu. Nikijaribu kufikiria kwa kipindi cha miaka yote ya ubunge kanifanyia nini ambacho atakapokuja tena kuomba kura atajivunia nacho na wananchi watafurahi kumwona tena, sikipati.Binafsi nimechoka! Nimechoka!
Umeme wakosekana masaa ishirini na matano na si mara moja kwa wiki!.Hakika haya ni masihara! Kwa hali hii lazima ningechoka tu!
Na nimeshachoka.
Ni kweli chama kimoja chashinda kwa halali miaka nenda uje? Kwa hali iliyopo, ni kweli watanzania ndio huwa wanakipigia kura! Ubabaishaji, rushwa, ufisadi,umasikini, kujengewa dhana ya kuwepo kwa amani lakini ni fujo na vurugu kila kukicha!Hivi, Yote haya kwa watanzania ni wimbo mzuri unaotufurahisha au ni nini?
Nimechoshwa! Nimechoshwa! Na kweli nimechoka.
Hivi,
kinachotuchosha watanzania ni, chama, mtu, watu au ni serikali? Au ni mfumo wa utawala?
Kwa vyovyote vile nimechoshwa na kweli nimeshachoka!
Kifaranga niliyetelekezwa, najitafutia kula mwenyewe, pori nijualo, kwa namna niwezayo. Kweli kwa hali hii maasi yatakwisha! Hali kama hizi si vichocheo tu vya matukio kama mauaji ya albino,wizi wa mabenki,uporaji, watu kuvamiwa majumbani na matukio mengine lukuki dhidi ya binadamu?
Binafsi nimechoka!
Saturday, September 5, 2009
Kutoka Bloguni.
Ni dhahiri kuwa mengi yaandikwayo na kuzungumzwa kwenye blogs zetu hayawafikii watu wengi ipasavyo.Wengi wanaosoma yanayoandikwa bloguni ni wale wenye internet access katika kompyuta na wenye uwezo wa kuzitumia pia.Wimbi la hali ngumu ya maisha lasabisha wachache kuweza kwenda kwenye internet cafe ili kuweza kutumia intenet.Mbali na niliyoyaeleza hapo juu, ufahamu wa blogs ni mdogo kwa jamii kubwa ya watu.
Ili kuhakikisha kuwa asilimia kubwa ya watu wanazifahamu blogs na angalao kuweza kupitia yaliyoandikwa(hata kama ni blogs chache) kuna jambo moja ambalo nalifikiria.Yawezekana hili lilishadokezwa lakini si vibaya nikilikumbushia.
Wazo hili ni la kubandika post fulani kwenye magazeti kutoka katika blog yoyote ilimradi tu post ile iwe ni ya kufunza au kuburudisha jamii.Si tu kwenye magazeti,hili lawezekana hata kwenye vituo vya televisheni na vituo vya redio,kwani naamini sehemu hizi zina huduma za internet.Kwa hiyo blog inaweza kufunguliwa na ikasomwa na hatimaye yaliyoandikwa kuwafikia watu wengi.Kwa utaratibu huu blogs zitafahamika na naimani kuwa wengi watahamasika ktk kuzipitia kwani kwa blog ambayo post yake itawekwa kwenye gazeti au kurushwa hewani kupitia radio au televisheni,naamini ile url nayo itarushwa vilevile ili kwa wanaotaka kujisomea kwa wakati wao waweze kufanya hivyo.
Naamini kuna waandishi wa habari wengi tu ambao wanamiliki blogs hivyo kwa namna moja ama nyingine wataweza kuliwekea mkazo na ufuatiliaji ili hatimaye liweze kufanikiwa.
Wewe kama mwanablog au mdau wa blogs utajisikiaje pale ambapo unasoma gazeti au wakati unaangalia televisheni au kusikiliza redio ukiona au kusikia kichwa hiki cha habari?
"kutoka bloguni"
"zisemavyo blogs"
"yanayojiri bloguni" n.k.
Ni wazo tu.
Ili kuhakikisha kuwa asilimia kubwa ya watu wanazifahamu blogs na angalao kuweza kupitia yaliyoandikwa(hata kama ni blogs chache) kuna jambo moja ambalo nalifikiria.Yawezekana hili lilishadokezwa lakini si vibaya nikilikumbushia.
Wazo hili ni la kubandika post fulani kwenye magazeti kutoka katika blog yoyote ilimradi tu post ile iwe ni ya kufunza au kuburudisha jamii.Si tu kwenye magazeti,hili lawezekana hata kwenye vituo vya televisheni na vituo vya redio,kwani naamini sehemu hizi zina huduma za internet.Kwa hiyo blog inaweza kufunguliwa na ikasomwa na hatimaye yaliyoandikwa kuwafikia watu wengi.Kwa utaratibu huu blogs zitafahamika na naimani kuwa wengi watahamasika ktk kuzipitia kwani kwa blog ambayo post yake itawekwa kwenye gazeti au kurushwa hewani kupitia radio au televisheni,naamini ile url nayo itarushwa vilevile ili kwa wanaotaka kujisomea kwa wakati wao waweze kufanya hivyo.
Naamini kuna waandishi wa habari wengi tu ambao wanamiliki blogs hivyo kwa namna moja ama nyingine wataweza kuliwekea mkazo na ufuatiliaji ili hatimaye liweze kufanikiwa.
Wewe kama mwanablog au mdau wa blogs utajisikiaje pale ambapo unasoma gazeti au wakati unaangalia televisheni au kusikiliza redio ukiona au kusikia kichwa hiki cha habari?
"kutoka bloguni"
"zisemavyo blogs"
"yanayojiri bloguni" n.k.
Ni wazo tu.
Saturday, August 29, 2009
Kuelekea uchaguzi mkuu.
Waonaje kama wananchi kwa pamoja wakikusanyika pamoja ili kujadili na kuchambua sera moja baada ya nyingine za wagombea watakaopita katika eneo lao ili kutambua kama sera hizo ni hai,zatekelezeka na zitawafaa na kuwafikisha mbali kimaendeleo kuliko kazi hii kufanywa na mtu mmoja mmoja?
Si tu kujadili sera bali hata kuwajadili viongozi wenyewe juu ya utendaji wao wa kazi,ufanisi,kama walishakuwa viongozi, walifanya nini na mambo kama hayo ambayo yataweza kutusaidia katika kuwapata viongozi bora na ambao ni wazalendo.
Naomba niliwasilishe hili kwenu na tulijadili kwa pamoja.
Si tu kujadili sera bali hata kuwajadili viongozi wenyewe juu ya utendaji wao wa kazi,ufanisi,kama walishakuwa viongozi, walifanya nini na mambo kama hayo ambayo yataweza kutusaidia katika kuwapata viongozi bora na ambao ni wazalendo.
Naomba niliwasilishe hili kwenu na tulijadili kwa pamoja.
Tuesday, August 25, 2009
Wito kwa wazazi/ walezi.
Inafahamika kuwa waislam wote wako katika mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan.Mfungo huu huwahusisha watu wazima na watoto.
Kwa upande wa watoto wale wanaosoma nimegundua kuna tatizo.Wanafunzi wanalala madarasani na wakiulizwa wanasema wamefunga.Wengine hulalamika kwa maumivu ya tumbo na hivyo kushindwa kuzingatia masomo ipasavyo.
Kimsingi wale wote wanaofunga wanatakiwa wawe na furaha wakati wote na taratibu za kawaida za kila siku hazitakiwi kukwama kwa kigezo cha kufunga.
Hivyo wazazi wawe makini na watoto wao,wawaelekeze yapi ya kuzingatia kwa wale wanaofunga.Pia wazazi lazima wawe makini kwani kuna watoto wasioweza kuhimili mfungo hivyo wazazi hawana budi kuwatambua na kuwaelekeza nini cha kufanya.
Nawatakia waislam wote mfungo mwema wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Kwa upande wa watoto wale wanaosoma nimegundua kuna tatizo.Wanafunzi wanalala madarasani na wakiulizwa wanasema wamefunga.Wengine hulalamika kwa maumivu ya tumbo na hivyo kushindwa kuzingatia masomo ipasavyo.
Kimsingi wale wote wanaofunga wanatakiwa wawe na furaha wakati wote na taratibu za kawaida za kila siku hazitakiwi kukwama kwa kigezo cha kufunga.
Hivyo wazazi wawe makini na watoto wao,wawaelekeze yapi ya kuzingatia kwa wale wanaofunga.Pia wazazi lazima wawe makini kwani kuna watoto wasioweza kuhimili mfungo hivyo wazazi hawana budi kuwatambua na kuwaelekeza nini cha kufanya.
Nawatakia waislam wote mfungo mwema wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Saturday, August 22, 2009
"Sidanganyikii!!"
Sio mimi nasema hivi bali ni kijana wa kike ambaye huwa anasikika kwenye vituo mbalimbali vya redio na pia kuonekana kwenye vituo vya televisheni.
Kijana huyu anasikika na kuonekana katika tangazo ambalo limethaminiwa/andaliwa na Umoja wa wanahabari wanawake Tanzania.Tangazo hili linawafundisha watoto wa kike hususani wa shule za msingi kukataa ofa zitolewazo na wanaume ambao lengo lao ni kuwahadaa KIMAPENZI.
Binafsi huwa napata maswali mengi kutoka ktk tangazo hili.
Huwa najiuliza kama neno "sidanganyiki" ni rahisi kutoka kwa mtoto wa kike ambaye hana malezi bora.Mbali na hilo kuna changamoto za umasikini zinazomkabili kijana huyu kama za kifedha, lishe bora,n.k. Sasa kwa hali hii "sidanganyiki" itaweza kutoka kweli na atamkaye atakuwa anamaanisha kweli? Kuna wakati miili yao inawatuma na kwa upande mwingine wako wanaume wakware na vijizawadi vidogovidogo.Kwa hali hii kijana huyu hawezi kushawishika na kuona kuwa ni neema juu yake kwani mbali na kutaka kutimiza matakwa ya mwili wake pia anajua atapata vizawadi?
Je, kijana huyu wa kike amewekewa uwezo gani wa kuweza kushinda matakwa ya mwili wake na kuweza kutamka "sidanganyiki" kutoka moyoni?
Ukweli ni kwamba si wote wenye uwezo wa kutamka neno hili na likiwa na maana kweli ya kwamba hawadanganyiki.Kwa nini kuna tofauti hizi?
Binafsi nadhani kinacholeta tofauti ni malezi ya watoto ktk familia na mazingira waliopo watoto hawa kwa ujumla.Vijana hawa lazima wajengewe misingi imara ya kukabiliana na changamoto na si kuwekewa "conditions" ambazo kuna mazingira ambayo ni vigumu sana kutumika na kufanikiwa kukwepa vishawishi.
Mwisho kabisa nasisitiza kwa kusema kuwa vijana hawa wajengewe misingi imara ya kuwawezesha kusema kuwa "hawadanganyiki" ili watambue kuwa wana maana gani kwa kusema hivyo na hatimaye "sidanganyikii!!" iwe ni ya kumaanisha kwelikweli.
Kijana huyu anasikika na kuonekana katika tangazo ambalo limethaminiwa/andaliwa na Umoja wa wanahabari wanawake Tanzania.Tangazo hili linawafundisha watoto wa kike hususani wa shule za msingi kukataa ofa zitolewazo na wanaume ambao lengo lao ni kuwahadaa KIMAPENZI.
Binafsi huwa napata maswali mengi kutoka ktk tangazo hili.
Huwa najiuliza kama neno "sidanganyiki" ni rahisi kutoka kwa mtoto wa kike ambaye hana malezi bora.Mbali na hilo kuna changamoto za umasikini zinazomkabili kijana huyu kama za kifedha, lishe bora,n.k. Sasa kwa hali hii "sidanganyiki" itaweza kutoka kweli na atamkaye atakuwa anamaanisha kweli? Kuna wakati miili yao inawatuma na kwa upande mwingine wako wanaume wakware na vijizawadi vidogovidogo.Kwa hali hii kijana huyu hawezi kushawishika na kuona kuwa ni neema juu yake kwani mbali na kutaka kutimiza matakwa ya mwili wake pia anajua atapata vizawadi?
Je, kijana huyu wa kike amewekewa uwezo gani wa kuweza kushinda matakwa ya mwili wake na kuweza kutamka "sidanganyiki" kutoka moyoni?
Ukweli ni kwamba si wote wenye uwezo wa kutamka neno hili na likiwa na maana kweli ya kwamba hawadanganyiki.Kwa nini kuna tofauti hizi?
Binafsi nadhani kinacholeta tofauti ni malezi ya watoto ktk familia na mazingira waliopo watoto hawa kwa ujumla.Vijana hawa lazima wajengewe misingi imara ya kukabiliana na changamoto na si kuwekewa "conditions" ambazo kuna mazingira ambayo ni vigumu sana kutumika na kufanikiwa kukwepa vishawishi.
Mwisho kabisa nasisitiza kwa kusema kuwa vijana hawa wajengewe misingi imara ya kuwawezesha kusema kuwa "hawadanganyiki" ili watambue kuwa wana maana gani kwa kusema hivyo na hatimaye "sidanganyikii!!" iwe ni ya kumaanisha kwelikweli.
Subscribe to:
Posts (Atom)
