Posts

Math Activity: Proving the SAS Congruence theorem

Image
This activity is based on Tanzanian Mathematics Syllabus for Secondary Schools. As a student, you are supposed to perform a series of tasks to develop an understanding of congruence of figures as well as proving the SAS congruence theorem. Proceed as follows:  1.  You are provided with shapes of different size as those shown in the figure below. Use any means of       your choice, sort out figures which are exactly the same. Give reasons.           2.      For the group of same figures, take two sets of figures and measure their angles and sides and draw a conclusion about your observation. 3.      Repeat task 3 but this time, use one figure from each group. What is your observation? 4.      Based on findings in tasks 3 and 4, what properties make the figures same or different? 5.      What is the term used to describe figures which are exactly the same? What are common properties of such figures? 6.      Use different math resources such as books and internet to confirm your

Namna ya Ujifunzaji ni Moja ya Changamoto kuu ya Elimu Yetu.

Image
Mwalimu Hottish wa Shule moja huko Ghana Akichora Kitumizi cha Microsoft Word kama namna ya kuwasaidia wanafunzi wake kujifunza. Picha kwa hisani ya www.MillardAyo.com Mjadala wa kujadili mustakabali wa Elimu yetu umeitishwa. Bila shaka ni kutokana na mwenendo usioridhisha wa elimu yetu.  Elimu yetu inaonekana kutokukidhi mahitaji ya watanzania na Taifa kwa ujumla. Hata hivyo, kabla ya kufika mbali, wadau wa elimu-walimu, wanafunzi, wazazi, raia, viongozi, n.k wanafahamu bayana kuhusu matarajio ya elimu inayotolewa? Kwa mini tunasema   elimu yetu imezorota? Wanafunzi kufeli sana? Mazingira ya kufundishia na kujifunzia kuwa magumu (sana)? Tunahitaji elimu itusaidie kufika wapi kama watanzania na kama Taifa?Pengine maswali haya yabaki kama sehemu ya kuchochea mjadala wa wa kitaifa kuhusu elimu nchini kwetu.  Makala haya yanalenga kushirikisha uzoefu wangu wa darasani na kuonesha angalao moja ya maeneo ambayo, yakifanyiwa kazi vizuri, yanaweza kuifanya elimu yetu ikapigiw

Kubadilika kwa Mitaala: Walimu na Wanafunzi Wabadilike kwa Namna Gani? Sehemu ya Pili.

Image
Picha kutoka Mtandaoni na kuboreshwa na mwandishi wa Makala haya. Katika makala iliyotangulia, nilijadili mambo makuu mawili ambayo walimu na wanafunzi wanapaswa kuyafanya ili kuendana na mfumo wa ufundishaji unaomzingatia mwanafunzi. Mamo haya mawili ni wajibu wa mwalimu na mwanafunzi na malengo ya maudhui yanayofundishwa. Makala haya yanalenga kuendelea kujadili namna nyingine tatu zinazoweza kuzingatiwa na walimu na wanafunzi ili kufanikisha utekelezaji wa mitaala inayomzingatia mwanafunzi. Kwenye makala haya, tutaaangalia wajibu wa kujifunza, nafasi ya mwalimu na mwanafunzi kuhusu masuala ya ujifunzaji na malengo ya upimaji wa mwanafunzi. Wajibu wa Kujifunza.  Wajibu wa kujifunza ni hali ya utayari wa mwanafunzi kushiriki kwenye mchakato wa ujifunzaji bila kulazimishwa ama kushurutishwa. Hali ilivyo sasa, wanafunzi wanafahamu wajibu wa mwalimu ni kuleta maarifa darasani na wajibu wa wanafunzi ni kumsikiliza mwalimu na kuandika nukuu.  Katika mfumo huu, mwalimu ndiy

Kubadilika kwa Mitaala: Walimu na Wanafunzi Wabadilike kwa Namna Gani?

Image
Kila mwanafunzi anajituma wakati wa kujifunza katika harakati za kufikia malengo yao ya ujifunzaji. Picha: Mwandishi wa makala Kama mnakumbuka, kati ya mwaka 2005 na  2007 yalitokea mabadiliko ya mitaala, hususani kwa shule za msingi, sekondari na vyuo vya Ualimu. Kulikuwa na msemo uliovuma sana wa "muhamo wa ruwaza" au "paradigm shift" kwa kiingereza. Ruwaza ni mfumo au imani inayomuwezesha mtu kutekeleza jambo fulani kulingana na matakwa na taratibu fulani zinazofahamika. Kwenye ufundishaji, iliaminika kuwa mitaala yetu ilikuwa ya mfumo unaomuona mwalimu kama chanzo cha maarifa na mwanafunzi kama pipa linalosubiri kujazwa tu maarifa. Mitaala mipya inaaminika kuwa ya ruwaza tofauti, ndio maana mabadiliko haya yakaitwa ya kuhama kwa ruwaza. Namna mitaala ilivyoandikwa na namna ya kuitekeleza ni miongoni mwa mabadiliko haya. Kwa mfano, mabadiliko haya yalipelekea maandalio ya masomo yawe na kipengele cha upimaji kwa kila hatua ya somo. Pia, zimependekezw

Popular posts from this blog

Mambo Makuu Manne ya Kuzingatia ili Kufanya Upimaji Endelevu Wenye Tija

Mambo Muhimu ya Kuzingatia Katika Kuboresha na Kuongeza Ufanisi wa Shule.

Kubadilika kwa Mitaala: Walimu na Wanafunzi Wabadilike kwa Namna Gani?