Posts

Showing posts from February, 2017

Juhudi Binafsi na Ndoto ya Mafanikio: Chachu ya Ufaulu wa Wanafunzi 10 Bora Matokeo ya Kidato cha Nne 2016

Image
                                               Picha na Mwandishi wa Makala haya Shule nyingi za serikali hususani za kata, zinafahamika kwa kukosa miundombinu rafiki ya kufundishia na kujifunzia.   Katika kutatua changamoto hii, zipo juhudi kadhaa ambazo zimefanyika ikiwa ni pamoja na kuanzisha kampeni ya kuhakikisha kila shule inakuwa na madawati ya kutosha. Hata hivyo, wakati kampeni hii ikiendelea, kuna baadhi ya shule zimeripotiwa kupungukiwa na madarasa ya kujifunzia.  Kwa upande mwingine, shule zinazomilikiwa na watu binafsi, nyingi zinafahamika kuwa na mazingira bora ya kufundishia na kujifunzia. Sambamba na hilo, shule hizi zimekuwa makini kuhakikisha wanafunzi wanaosajiliwa ni wale wenye uwezo mzuri darasani. Hili huhakikishwa kwa kuwachuja wanafunzi kila wanapomaliza kidato kimoja au muhula. Hii ina maana kuwa, vijana wanaofikia kufanya mtihani wa kidato cha nne au cha pili ni wale waliojihakikishia kufanya vizuri.  Matokeo ya kidato cha Nne kwa mwaka 2016

Popular posts from this blog

Mambo Makuu Manne ya Kuzingatia ili Kufanya Upimaji Endelevu Wenye Tija

Mambo Muhimu ya Kuzingatia Katika Kuboresha na Kuongeza Ufanisi wa Shule.

Kubadilika kwa Mitaala: Walimu na Wanafunzi Wabadilike kwa Namna Gani?