Walimu, Ninyi ndio Mnaojifunza, Wanafunzi wenu ni Wapokea Taarifa tu
Picha kwa hisani ya www.jiandae.wordpress.com Kuna msemo usemao, kati ya anayefundisha na anayefundishwa, anayejifunza zaidi ni yule anayefundisha/ elekeza. Msemo huu una ukweli kwa kuwa, anayefundisha hujiandaa kwa kila hali na pia kupata fursa ya kutumia kile alichojifunza kwa kuelekeza wenzake. Msemo huu bila shaka, chanzo chake ni aina ya ufundishaji wa muda mrefu uliozoeleka mashuleni. Kwamba, mwalimu ndiye anayepaswa kusoma kwa kina na kisha kuwaeleza wanafunzi dhana ya yale aliyoyasoma. Kimsingi, mwalimu anatoa taarifa ya alichojifunza kile wanafunzi wanachopaswa kukijifunza. Bila shaka unaweza ukashangazwa au kupata mshtuko, lakini hali halisi ndio hii. Kabla ya kufundisha, mwalimu anapaswa kujiandaa na somo. Kwa mtazamo wa ufundishaji wa walimu wengi, jukumu lao kubwa ni kujisomea ili wapate uelewa wa kutosha kuhusu kile wanachopaswa kuk