Namna Walimu Wanavyoweza Kuboresha Ufundishaji Kwa Kutumia TEHAMA
Picha ya sehemu ya ndani ya moyo kutoka kwenye moja ya Video inayoelezea mfumo wa mzunguko wa damu Kwa kipindi cha miaka ya 2011 hadi 2013 nilikuwa mmoja wa wawezeshaji wa mradi wa kuwawezesha walimu wa shule za sekondari kutumia Teknologia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kwenye mchakato wa ufundishaji na ujifunzaji. Mradi huu ujulikanao kama SME (Science, Maths and English)-ICT Project , ulikuwa unatekelewa na Wizara ya Elimu na mafunzo ya Ufundi (MoEVT). Mradi huu ulilenga masomo ya sayansi ambayo ni Biolojia, Kemia na Fizikia. Masomo mengine yalikuwa ni Kiingereza na hisabati. Kwa mujibu wa tafiti, masomo haya yalionekana wanafunzi wanafeli sana, na hivyo moja ya namna ya kukabiliana na changamoto hii ilikuwa ni kuanzishwa kwa mradi huu wa majaribio. Walimu walifundishwa namna ambavyo wangeweza kutumia kompyuta pamoja na vifaa vingine kama projekta kwenye ufundishaji na ufunza