Posts

Showing posts from March, 2015

Shairi: Kilio cha Albino

Image
                   Picha kutoka Yahoo news Kisa ni mbovu imani, Ndugu zetu mwawaua, [ Amir Kulanteni] Mwamuabudu shetani, Mmezitupa sheria, Twapita tu duniani, Kifo chaja kwenu pia, Kilio cha Albino, Hivi kweli tunajali? Wenye dhima mwafanyani? Uhai kutulindia, Wananchi mashakani, Nyie kiguu na njia, Mara mpo marekani, Sisi huku tunalia, Kilio cha Albino, Hivi kweli tunajali? Mwaiba mabilioni, Mwashindwa kututetea, Ni kama watu usoni, Moyoni mwatumendea, Ni kama tu hayawani, Imani zimepotea, Kilio cha Albino, Hivi kweli tunajali? Vitendo vyangoja nini?, Matamko tu mwatoa, Ndugu zetu kaburini, Hamuioni kadhia, Matendo ya kishetani, Nyie mwayakaushia, Kilio cha Albino, Hivi kweli tunajali? Twendeni makanisani, Tuombe huku twalia, Twendeni misikitini, Tuzisome kali dua, Mungu na awalaani, Motoni aje watia, Kilio cha Albino, Hivi kweli tunajali?    Amiri wa Kulanteni , Beti umezipatia,        [Mutabazi Muta Mutabe] Ujumbe zimesheheni, Saluti na

TPACK: Moja ya Maarifa Muhimu kwa Walimu

Image
  Picha imetumiwa kwa ruhusa kutoka http://tpack.org      TPACK ikiwa ni kifupisho cha Technological Pedagogical Content Knowledge, ni n adharia inayolenga kutoa ufafanuzi wa ujuzi anaopaswa kuufahamu mwalimu ili aweze kutumia TEHAMA kwa ufasaha katika ufundishaji wake. Modeli hii inamkumbusha mwalimu kuhusu aina ya ujuzi anaotakiwa kuwa nao, ukiwamo wa kutumia Tehama katika ufundishaji. Kwa mujibu wa modeli hii, ujuzi huu upo katika sehemu kuu tatu ambazo ni Ujuzi wa ufundishaji (pedagogy), Ujuzi wa Maudhui ya somo (content knowledge) na Ujuzi wa tekinologia (Technological Knowledge) unaokusudiwa kutumiwa kwenye ufundishaji.   Hata hivyo, nadharia ya TPACK inaenda mbali zaidi kwa kuonesha pia namna ujuzi huu niliotangulia kuutaja unavyoingiliana na kutegemeana. Hii ni kusema, mwalimu akiwa na ujuzi wa kufundisha halafu hayajui vyema maudhui ya somo, ni sawa na kazi bure. Itamwia vigumu kufanikisha ufundishaji.  Hali kadhalika,  kama mwalimu anauelewa mpana wa maudhui

Popular posts from this blog

Mambo Makuu Manne ya Kuzingatia ili Kufanya Upimaji Endelevu Wenye Tija

Mambo Muhimu ya Kuzingatia Katika Kuboresha na Kuongeza Ufanisi wa Shule.

Kubadilika kwa Mitaala: Walimu na Wanafunzi Wabadilike kwa Namna Gani?