Posts

Showing posts from February, 2011

Soko la Magulioni-Singida Mashariki

Image
Kati ya sehemu ambazo wananchi wake wanahatarisha maisha yao, basi ni hapa katika soko hili liitwalo MAGULIONI ambalo lipo eneo maarufu liitwalo Njia panda ya Makiungu pembezoni mwa barabara ya Singida-Manyara. soko hili huwa kila siku ya Jumamosi na husheheni vitu vya kila aina kuanzia mboga mboga, nguo, kuku, miwa, vyungu, vyakula mbali mbali vikiwemo viazi vitamu vilivyopikwa na ambavvo havijapikwa, majembe n.k Kiujumla, halitofautiani na masoko mengine ambayo ulishawahi kuyaona. Mbali na upatikanaji wa vitu mbali mbali nilivyojitahidi kuvitaja, lakini pia, kila Jumamosi idadi kubwa ya watu hulitegemea sana soko hili kwa kitoweo cha nyama: kuanzia ya ng'ombe hadi ya mbuzi. Walaji wa nyama hizi kwa hakika wapo katika hatari kubwa sana kwani kulingana na uchunguzi wangu niligundua kuwa hakuna dakitari wa kuangalia uhalali wa matumizi ya nyama hizo, machinjio duni na pia sehemu za kuuzia nyama hizo ni hatari kabisa kwa afya za walaji. Picha hapa chini zinaonesha baadhi ya mabu

Popular posts from this blog

Mambo Makuu Manne ya Kuzingatia ili Kufanya Upimaji Endelevu Wenye Tija

Mambo Muhimu ya Kuzingatia Katika Kuboresha na Kuongeza Ufanisi wa Shule.

Kubadilika kwa Mitaala: Walimu na Wanafunzi Wabadilike kwa Namna Gani?