Posts

Showing posts from April, 2010

Lijue na hili

Image
Wakati mwingine wanyama(wafugwao majumbani na hata wale wa kwenye hifadhi) wanapopatwa na matatizo(mfano ugonjwa), inakuwa vigumu kutambua. Kwa kiasi kikubwa unahitajika utaalamu na uzoefu ili kuweza kugundua mapema kabla hali haijakuwa mbaya na hata kupelekea kumpoteza mnyama. Je, wafahamu dalili ya awali kabisa pale ng'ombe anapokuwa amepatwa na ugonjwa fulani? Kama unajua,ni vema,utanisadia kuboresha,na kama ulikuwa hujui,basi, ni wakati wako mzuri wa kujifunza. Kwa kawaida ng'ombe mwenye afya njema pua yake huwa na unyevunyevu wakati wote. Kwa ng'ombe ambaye ameanza au anayeshambuliwa na ugonjwa, pua yake huwa kavu kabisa. Kwa hiyo pindi uonapo pua ya ng'ombe imekuwa kavu, chukua hatua za haraka za kumuita mtaalamu kwa uchunguzi zaidi na matibabu.

Uyoga huu wa Ajabu!

Image
Dunia ina mengi ya kufurahisha na pia ya kustaajabisha kama sio kushangaza. Juzi nikiwa nyumbani nimejipumzisha chini ya mti wenye kivuli kizuri huku nikipata upepo mwanana,ghafla nilianza kuhisi harufu kama ya mzoga(mnyama aliyekufa). Harufu ile iliniwewesesha kwa kweli na ndipo iliponilazimu kuanza kufuatilia huo mzoga ambao nilijua lazima utakuwa ni wa mnyama tu. Nilifuatilia kwa makini katika eneo lile na kwa msaada wa kundi la inzi(ati wanasema inzi wana busara sana,huwa wako makini sana kutujulisha pale penye mzoga au kinyesi ili tusikanyage au kusogea karibu) niliweza kuona ulipo mzoga huo. Nilisogea karibu pamoja na harufu kali ya mzoga. Kinyume na matarajio yangu, niliuona UYOGA unaostawi vizuri ndio huo hasa uliokuwa umezingirwa na nzi pale nchani. Niliona ni vema niupige picha na kisha nikauondoa nikaenda kuutupa mbali na harufu ile ikawa imetoweka. Siku tatu baadae nikaihisi harufu ile na cha kwanza nilichofanya ni kwenda eneo lile na kukagua kama kuna uyoga wa aina ile. Kw

Popular posts from this blog

Mambo Makuu Manne ya Kuzingatia ili Kufanya Upimaji Endelevu Wenye Tija

Mambo Muhimu ya Kuzingatia Katika Kuboresha na Kuongeza Ufanisi wa Shule.

Kubadilika kwa Mitaala: Walimu na Wanafunzi Wabadilike kwa Namna Gani?